Accueil Podcasts Gurudumu la Uchumi
Gurudumu la Uchumi

Gurudumu la Uchumi

RFI Kiswahili 24 Épisodes sept. 9, 2026

Fahamu masuala kadha wa kadha kuhusu uchumi kama vile, namna ya kupambana na umaskini, mfumuko wa bei, kushamiri kwa matumizi ya dola na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa nchi za Afrika. Mada hizi zinafanyiwa utafiti wa kina na zinazungumzwa kwa lugha rahisi inayoeleweka ili kukufanya uelewe na usichoke kusikiliza.

Épisodes

Maisha mapya: Jinsi akina mama vijana wanavyobadilisha ujuzi kuwa fursa
Maisha mapya: Jinsi akina mama vijana wanavyobadilisha ujuzi kuwa fursa sept. 9, 2026 00:10:05 Nchini Kenya, suala la mimba za utotoni ni changamoto. Kwa mujibu wa ofisi ya Takwimu ya taofa nchini Kenya kupitia utafiti wa mwaka 2022 asilimia 15 ya wasichana wenye umri wa miaka 15 hadi 19 walikuwa wamewahi kupata ujauzito. Katika makala ya Gurudumu la Uchumi wiki hii, tunaangazia namna akina mama hawa wanavyogeuza ujuzi, juhudi na fursa za kiuchumi kuwa njia ya kujitegemea na kuwajengea wato
Umeme unaweza kuwa injini ya ukuaji wa uchumi Afrika Mashariki?
Umeme unaweza kuwa injini ya ukuaji wa uchumi Afrika Mashariki? août 26, 2026 00:10:04 Wikendi iliyopita, Tanzania ilizundua rasmi Mradi wa Umeme wa Maji wa bwawa la Julius Nyerere, lenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115. Mradi huu, uliogharimu takribani shilingi trilioni 7.45 za Tanzania sawa na karibu dola za Marekani bilioni 2.9, unaongeza kwa kiasi kikubwa uwezo wa Tanzania kuzalisha umeme. Katika Makala ya Gurudumu la uchumi wiki hii, tunajiuluza Je, megawati hizi zitageuka ku
Goma: Wanawake wapambana na umaskini licha ya changamoto za usalama.
Goma: Wanawake wapambana na umaskini licha ya changamoto za usalama. août 19, 2026 00:10:03 Msikilizaji katika mazingira ambayo migogoro na changamoto za kiuchumi zimeathiri maisha ya kila siku ya wananchi, wanawake wengi wamekuwa wakitafuta njia mbadala za kujipatia kipato na kuendesha familia zao.Hali hii inashuhudiwa katika mji wa Goma, mashariki mwa DRC, ambako baadhi ya wanawake wamegeukia ufugaji wa kuku kama njia ya kujikimu, hasa baada ya shughuli za baadhi ya taasisi za kifedha
Je, Nchi Inaweza Kuendelea Bila Dira ya Maendeleo?
Je, Nchi Inaweza Kuendelea Bila Dira ya Maendeleo? août 12, 2026 00:10:01 Msikilizaji taifa linaweza kuishi siku moja baada ya nyingine bila kujua linaelekea wapi. Lakini taifa linalotaka kujenga uchumi imara, ajira bora na maisha bora kwa wananchi wake, linahitaji zaidi ya mipango ya leo, kwa kifupî linahitaji dira. Kwenye makala ya wiki hii tunaangazia dira ya taifa ni nini.
Sehemu ya Pili: Hatifungani ni nini na kwanini inakuhusu
Sehemu ya Pili: Hatifungani ni nini na kwanini inakuhusu août 5, 2026 00:10:03 Mara kadhaa tumesikia serikali zetu zikitangaza kuwa zinauza hati fungani za Serikali za muda mfupi na muda mrefu, yaani Government Bonds na Treasury bill, serikali zikikusanya mabilioni ya fedha kutoka kwa wawekezaji. Sasa je, hatifungani ni nini? Je, mwananchi wa kawaida anaweza kuwekeza?
Hatifungani za serikali na hazina: Kwa nini zinahusu kila mwananchi?
Hatifungani za serikali na hazina: Kwa nini zinahusu kila mwananchi? juil. 29, 2026 00:10:01 Mara kadhaa tumesikia serikali zetu zikitangaza kuwa zinauza hati fungani za Serikali za muda mfupi na muda mrefu, yaani Government Bonds na Treasury bill, serikali zikikusanya mabilioni ya fedha kutoka kwa wawekezaji. Sasa je, hatifungani ni nini? Je, mwananchi wa kawaida anaweza kuwekeza?
Migogoro ya kimataifa inavyoathiri uchumi wa wananchi Afrika
Migogoro ya kimataifa inavyoathiri uchumi wa wananchi Afrika juil. 22, 2026 00:10:03 Katika Makala haya hivi leo tunajadili uhusiano kati ya siasa za kimataifa na uchumi wa wananchi wa Afrika, mara yingi tunasikia taarifa za vita, migogoro ya kisiasa au mivutano kati ya mataifa makubwa kama Urusi na Ukraine, Mashariki ya Kati, au migogoro inayovuruga usafirishaji wa bidhaa duniani. Kuzungumzia hili, hivi leo nimemualika Safari Fungo, mtaalamu wa masuala ya uchumi, utangamano wa ki
Sarafu za kidijitali ‘Cryptocurrency’ uwekezaji wa kisasa wenye fursa na hatari
Sarafu za kidijitali ‘Cryptocurrency’ uwekezaji wa kisasa wenye fursa na hatari juil. 15, 2026 00:09:41 Katika miaka ya hivi karibuni, sarafu za kidijitali maarufu kama cryptocurrency zimezidi kuvutia watu wengi duniani. Wapo waliopata faida kubwa, lakini pia wapo waliopoteza fedha nyingi kutokana na kushuka kwa thamani ya sarafu hizo. Leo katika Makala ya Gurudumu la Uchumi, tunajiuliza: Je, sarafu za kidijitali ‘cryptocurrency’ ni uwekezaji wa kweli, au ni uwekezaji wenye hatari kubwa ambao watu w
Kodi na Maendeleo: Je, tunapata thamani ya kodi tunazolipa?
Kodi na Maendeleo: Je, tunapata thamani ya kodi tunazolipa? juil. 8, 2026 00:09:56 Katika makala ya Gurudumu la Uchumi hivi leo, tunajadili nafasi ya kodi katika maendeleo ya uchumi, umuhimu wa kulipa kodi, na jinsi serikali na wananchi wanavyoweza kushirikiana kujenga uchumi imara na wenye manufaa kwa wote.
Je, kukopa kunasaidia ukuaji wa uchumi au kunaleta hatari za siku zijazo?
Je, kukopa kunasaidia ukuaji wa uchumi au kunaleta hatari za siku zijazo? juin 24, 2026 00:10:04 Msikilizaji nchi nyingi za Afrika Mashariki zimeendelea kukopa ili kufadhili maendeleo, na huku wadau wengine wakisema mikopo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi, Wengine wanaonya kuwa madeni yanapoongezeka kupita kiasi, serikali hulazimika kutumia fedha nyingi kulipa madeni hayo badala ya kuboresha huduma muhimu kama vile afya, elimu na ajira. Katika Makala ya Gurumu la Uchumi hivi leo, tunauliza: Je,
Kutoka taslimu hadi kidijitali: Namna simu zinavyobadili mfumo wa malipo Afrika
Kutoka taslimu hadi kidijitali: Namna simu zinavyobadili mfumo wa malipo Afrika juin 10, 2026 00:10:03 Ufanyaji biashara na utumaji wa fedha kwa njia ya simu za kiganjani barani Afrika unakua kwa kasi, pochi za simu zimerekodi takriban asilimia 19 ya uingiaji wa pesa kwenye eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara, huku wastani wa gharama ya utumaji pesa ukishuka hadi karibu asilimia 3.54 hii ni kwa mujibu wa benki ya dunia. Kwanye Makala ya Gurudumu la uchumi wiki hii, tunaangazia matumizi ya telknoloj
Sekta ya maua Kenya yatikiswa na gharama na kuyumba kwa masoko ya kimataifa
Sekta ya maua Kenya yatikiswa na gharama na kuyumba kwa masoko ya kimataifa juin 4, 2026 00:09:55 Msikilizaji Sekta ya maua nchini Kenya, ambayo kwa muda mrefu imekuwa miongoni mwa nguzo muhimu za uchumi na chanzo kikuu cha mapato ya fedha za kigeni, ikiingizia nchi zaidi ya dola bilioni moja za Marekani kila mwaka, sasa inakabiliwa na changamoto zinazotia wasiwasi kuhusu mustakabali wake.

Recommandé